Wasiliana nasi | MMM | Barua Pepe |

Afya ya jamii

Jifunze njia za kujikinga na maambukizi ya Ebola.

Njia za kujikinga na ugonjwa huu ni :

  • Epuka kusalimiana kwa kushikana mikono au kukumbatiana
  • Epuka kugusa damu, matapishi, mkojo, kinyesi, kamasi, mate, machozi na maji maji mengine yanayotoka mwilini mwa mtu mwenye dalili za ugonjwa huu
  • Epuka kugusa au kuosha maiti ya mtu aliyekufaakiwa na dalili za ebola badala yake toa taarifa kwa uongozi wa serikali ili wasimamie taatibu za mazishi
  • Epuka kutumia nguo, shuka, blanketi, kitanda nagodoro za mtu aliyeambukizwa ugonjwa, toa taarifa kwenye ofisi za serikali ya eneo husika
  • Kwa kuwa ugonjwa huu pia huambukizwa kwa njia ya kujamiiana, epuka kuwa na mpenzi zaidi ya mmoja
  • Nawa mikono kwa maji yanayotiririka na sabuni mara unapomtembelea mgonjwa hospitalini au kumhudumia nyumbani
  • Epuka kugusa wanyama kama vile popo, nyani, sokwe, tumbili na swala au mizoga ya wanyama
  • Zingatia ushauri na maelekezo yanayotolewa na wataalamu wa afya na viongozi wa serikali.
  • Wahi kituo cha kutolea huduma za afya uonapo dalili za ugonjwa wa Ebola
  • Toa taaifa mapema kwa watoa huduma za afya uonapo mtu mwenye dalili za ugonjwa wa Ebola au kifo
  • Zingatia usafi binafsi pamoja na usafi wa mazingira yako.



HEDHI - CUP.

HEDHI CUP-SWAHILI-BERNO.pptx